8 Taji mvikeni


1. Taji mvikeni,
Taji nyingi tena,
Kondoo mwake kitini,
Bwana wa mabwana;
Nami tamsifu
Alikufa kwangu,
Ni mfalme mtukufu,
Mkuu wa Mbingu.
 
2. Taji mvikeni
Mwana wa bikira;
Anazovaa kichwani
Aliteka nyara;
Shiloh wa wanabii,
Mchunga wa watu,
Shina na tanzu vya Yese,
Wa Bethilehemu.
 
3. Taji mvikeni
Bwana wa mapenzi;
Jeraha zake ni shani
Ni vito vya enzi,
Mbinguni hakuna
Hata malaika
Awezaye kuziona
Pasipo kushangaa. 

Comments

Popular posts from this blog

23 Ni salama rohoni mwangu

7 Ni tabibu wa karibu

16 Kumtegemea Mwokozi