7 Ni tabibu wa karibu


1. Ni tabibu wa karibu;
Tabibu wa ajabu;
Na rehema za daima;
Ni dawa yake njema.
 
Imbeni, malaika,
Sifa za Yesu Bwana;
Pweke limetukuka
Jina lake Yesu.
 
2. Hatufai kuwa hai,
Wala hatutumai,
Ila kweli yeye ndiye
Atupumzishaye.
 
3. Dhambi pia na hatia
Ametuchukulia;
Twenendeni na amani
Hata kwake Mbinguni.
 
4. Huliona tamu jina
La Yesu Kristo Bwana,
Yuna sifa mwenye kufa
Asishindwe na kufa.
 
5. Kila mume asimame,
Sifa zake zivume;
Wanawake na washike
Kusifu jina lake.
 
6. Na vijana wote tena,
Wampendao sana
Waje kwake wawe wake
Kwa utumishi wake. 

Comments

Popular posts from this blog

23 Ni salama rohoni mwangu

16 Kumtegemea Mwokozi