65 Safari


1. Katika safari yetu
Kwenda Mbinguni
Tusiishe siku zetu
Usingizini. 
 
Ng’oani! Tujifungeni,
Twende zetu juu!
Kristo ndiye kiongozi;
Tusihofu tu. 
 
2. Atwekwe badala yetu,
Mwenyewe Bwana;
Yesu kiongozi wetu
Atapokea.
 
3. Kisimani, maji tele,
Maji mazima!
Maji hayo,
Ya milele
Yana neema.
 
4. Njiani miiba mingi,
Yatuumiza;
Hofu na hatari nyingi,
Sana zakaza.
 
5. Kweli, njia ya Mbinguni
Ni ya mashaka;
Tuwe na Yesu njiani,
Mara hufika. 

Comments

Popular posts from this blog

23 Ni salama rohoni mwangu

7 Ni tabibu wa karibu

16 Kumtegemea Mwokozi