62 Bwana wa mabwana


1. Bwana wa mabwana,
Mwenye nguvu sana
Twakusihi:
Neno la milele
Na liende mbele,
Waongoke tele
Kwa Mwokozi. 
 
2. Tunaowaona
Wanavyopatana,
Kulipinga,
Hawataliweza
Neno, kulitweza:
Huwaje! Kucheza:
Na upanga?
 
3. Heri wajitunze
Ili wapatane,
Na Mwokozi;
Watafute sana,
Wapate kuona,
Yesu kuwa Bwana,
Mkombozi.
 
4. Mungu awaita
Wasije kukuta
Pigo lake;
Hakuona vyema
Wakose uzima,
Awape rehema,
Waokoke.
 
5. Mwenye utukufu
Tunamshukuru
Yeye pweke!
Nasifiwe sana,
Baba, naye Mwana,
Na wa tatu tena
Roho yake. 

Comments

Popular posts from this blog

23 Ni salama rohoni mwangu

7 Ni tabibu wa karibu

16 Kumtegemea Mwokozi