46 Twae wangu uzima


1. Twae wangu uzima,
Sadaka ya daima;
Twae saa na siku,
Zikutukuze huku. 
 
2. Twae mikono nayo
Ifanye upendavyo,
Twae yangu miguu
Kwa wongozi wako tu.
 
3. Twae sauti yangu,
Niimbe kwa Mungu tu;
Itwae na midomo,
Ijae neno lako.
 
4. Twae dhahabu pia,
Na yote ya dunia;
Twae yangu hekima,
Upendavyo tumia.
 
5. Nia itwae, Mungu,
Haitakuwa yangu;
Twae moyo; ni wako,
Uwe makazi yako.
 
6. Twae mapenzi yangu,
Sifa za moyo wangu;
Twae kabisa nafsi
Niwe wako halisi. 

Comments

Popular posts from this blog

23 Ni salama rohoni mwangu

7 Ni tabibu wa karibu

16 Kumtegemea Mwokozi