33 Dhambi ikikulemea


1. Dhambi ikikulemea,
Kwa Bwana rehema;
Hivi sasa tegemea
Neno la salama. 
 
Tegemea, tegemea,
akwita sasa.
Ni Mwokozi, ni
Mwokozi; amini sasa. 
 
2. Yesu amemwaga damu
Ya nyingi baraka;
Nawe sasa oga mumu
Zioshwamo taka.
 
3. Ni njia yeye hakika
Hwongoza rahani;
Usikawe kumshika,
Uwe barakani.
 
4. Karibu nawe wingie
Mwetu safarini,
Twende tukamwamkie,
Milele Mbinguni. 

Comments

Popular posts from this blog

23 Ni salama rohoni mwangu

7 Ni tabibu wa karibu

16 Kumtegemea Mwokozi