32 Yesu awakubali wakosa


1. Yesu awakubali,
Wakosa, wahalifu,
Wambieni wa mbali
Habari ya wokovu. 
 
Tangazeni kwa bidii,
“Akubali wakosa!”
Liwe neno dhahiri,
“Akubali wakosa!” 
 
2. Awakubali Bwana
Neno lake amini
Watu kila aina
Waje kwake tengoni.
 
3. Mimi ni safi moyo
Na mbele ya sharia,
Aliye safi roho
Kwake ilitimia.
 
4. Akubali wakosa;
Nami anikubali;
Alivyonitakasa
Mbinguni niwasili.

Comments

Popular posts from this blog

23 Ni salama rohoni mwangu

7 Ni tabibu wa karibu

16 Kumtegemea Mwokozi