84 Niwonapo mti bora

 
1. Niwonapo mti bora
Kristo aliponifia
Kwangu pato ni hasara
Kiburi nakichukia. 
 
2. Na nisijivune, Bwana
Ila kwa mauti yako;
Upuzi sitaki tena,
Ni chini ya damu yako.
 
3. Tangu kichwa hata nyayo,
Zamwagwa pendo na hamu,
Ndako pweke hamu hiyo,
Pendo zako zimetimia.
 
4. Vitu vyote vya dunia,
Si sadaka ya kutosha;
Pendo zako zinawia
Nafsi, mali, na maisha. 

Comments

Popular posts from this blog

23 Ni salama rohoni mwangu

7 Ni tabibu wa karibu

16 Kumtegemea Mwokozi