144 Mbele ninaendelea


1. Mbele ninaendelea,
ninazidi kutembea.
Maombi uyasikie,
Ee Bwana, unipandishe.
 
Ee, Bwana, uniinue,
Kwa imani nisimame;
Nipande milima yote,
Ee Bwana,
Unipandishe.
 
2. Sina tamani nikae,
Mahali pa shaka, kamwe;
Hapo wengi wanakaa,
Kuendelea naomba.
 
3. Nisikae duniani,
asumbuapo Shetani;
Natazamia mbinguni,
nitafika na amani.
 
4. Nataka nipandishwe juu,
Zaidi yale mawingu.
Nitaomba nifikishwe,
Ee Bwana unipandishe.

Comments

Popular posts from this blog

23 Ni salama rohoni mwangu

7 Ni tabibu wa karibu

16 Kumtegemea Mwokozi