161 Usiku uingiapo



1. Usiku uingiapo,
umwaze Mungu Mkuu,
aendeshaye dunia
kwa mwendo mtulivu.
 
2. Kwa nini wahangaika
usiku namchana?
Umtwishe huzuni yako
aliyekuumba.
 
3. Kwake haujapunguka
uwezo na msaada.
Atayatimiza yote
aliyoyaanza.
 
4. Ukamwachie kutenda
atakalo kwako!
Kwa hiyo ulale raha
na kufurahiwa.

Comments

Popular posts from this blog

23 Ni salama rohoni mwangu

7 Ni tabibu wa karibu

16 Kumtegemea Mwokozi