157 Kijito cha utakaso


 
1. Kijito cha utakaso
ni damu ya Yesu,
Bwana anao uwezo
kunipa wokovu
 
Kijito cha utakaso,
Nizame kuoshwa humo
Namsifu Bwana kwa hiyo
Nimepata utakaso
 
2. Viumbe vipya naona;
damu ina nguvu,
imeharibu uovu
ulionidhulumu
 
3. Naondoka kutembea
nuruni mwa mbingu,
Na moyo safi kabisa
kumpendeza Mungu.
 
4. Ni neema ya ajabu
kupakwa na damu;
na Bwana Yesu kumjua
Yesu wa Msalaba.


Comments

Popular posts from this blog

23 Ni salama rohoni mwangu

7 Ni tabibu wa karibu

16 Kumtegemea Mwokozi