157 Kijito cha utakaso
1. Kijito cha utakaso
ni damu ya Yesu,
Bwana anao uwezo
kunipa wokovu
Kijito cha utakaso,
Nizame kuoshwa humo
Namsifu Bwana kwa hiyo
Nimepata utakaso
2. Viumbe vipya naona;
damu ina nguvu,
imeharibu uovu
ulionidhulumu
3. Naondoka kutembea
nuruni mwa mbingu,
Na moyo safi kabisa
kumpendeza Mungu.
4. Ni neema ya ajabu
kupakwa na damu;
na Bwana Yesu kumjua
Yesu wa Msalaba.
Comments
Post a Comment